TAMISEMI YARIDHISHWA NA KASI YA UJENZI MADARASA TARIME VIJIJINI,NAIBU WAZIRI DAVID SILINDE ATOA PONGEZI ZA DHATI


 Naibu Waziri Ofisi ya Rais – TAMISEMI- Elimu, David Silinde leo Novemba 27, 2022 amekagua maendeleo ya ujenzi wa vyumba vya madarasa ya shule za sekondari katika Halmashauri ya Wilaya ya Tarime mkoani Mara na kutaka kasi aliyoikuta iendelee ili yakamilike kwa wakati.

“Ninatoa rai kasi hii iendelee, madarasa yote katika halmashauri hii yakamilike kwa wakati na mtoe taarifa mkoani ili nao watuletee, kwa sababu na sisi tuna lengo la kumkabidhi Rais madarasa yote 8,000 yakiwa yamekamilika,” Silinde alisema mara baada ya kukagua ujenzi wa madarasa mawili katika Shule ya Sekondari Nyantira.

Amesema yupo katika ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa vyumba vya madarasa maeneo mbalimbali nchini, kutokana na fedha zilizotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ili kuwezesha wanafunzi wote watakaochaguliwa kuingia kidato cha kwanza mwaka 2023 wanapata nafasi.

“Rais ametoa fedha za madarasa 8,000 nchini ili watoto wote wapate nafasi kama alivyofanya mwaka jana [2021],” Naibu Waziri David Silinde amesema na kuwataka viongozi husika kuhakikisha yanakamilika kwa wakati.

Comments

Popular posts from this blog

Mkuu wa Mkoa wa Mara Awapongeza Halmashauri ya Wilaya ya Tarime