MAAGIZO YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, DKT. JOHN POMBE JOSEPH MAGUFULI ALIYOYATOA WAKATI WA ZIARA YAKE WILAYANI TARIME YATEKELEZWA KWA KISHINDO




Hatimaye Wakazi 1,639 wa Vijiji vya Matongo na Nyabichune katika eneo la Nyamongo Wilayani Tarime Mkoa wa Mara wamelipwa fidia ya jumla ya Shilingi Bilioni 33 baada ya kusubiri kwa kipindi cha miaka 10.

Fidia hiyo imelipwa Mei 20, 2020 na Mgodi wa  Barrick North Mara  ikiwa  Utekelezaji wa Maagizo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli aliyoyatoa wakati wa ziara yake Wilayani Tarime  ambapo alitaka suala hilo ikiwemo la uchafuzi wa mazingira yamalizwe haraka.

Akizungumza wakati wa Ufunguzi wa utoaji fidia  na Ugawaji wa Cheki kwa Wakazi hao waliopisha maeneo yao kwa ajili ya uendelezaji wa shughuli za mgodi huo, Waziri wa Madini Doto Biteko amewahakikishia wote wenye haki ya kulipwa fidia hiyo kuwa watalipwa fedha zao.

Aidha, ametoa pongeza kwa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi na kueleza kuwa Wizara hiyo ilifanya kazi usiku na mchana kuhakikisha inamaliza mgogoro wa fidia uliokuwepo baina ya wananchi na mgodi huo.

Comments

Popular posts from this blog

Mkuu wa Mkoa wa Mara Awapongeza Halmashauri ya Wilaya ya Tarime