Mkuu wa Mkoa wa Mara Awapongeza Halmashauri ya Wilaya ya Tarime

Tarime inapendeza



MKUU WA MKOA WA MARA AWAPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA TARIME KWA KUTII AGIZO HARAKA LA MHE DK. JOHN POMBE JOSEPH MAGUFURI RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA KWA KUHAMIA NYAMWANGA.
Kufuatia agizo la Rais wa awamu ya tano Dk.John Pombe Joseph Magufuri kuagiza halmashauri zote kuhama mjini na kwenda maeneo ya vijijini (maeneo yao ya utawala), alipokuwa katika ziara ya kikazi  mkoani Rukwa katika wilaya ya sumbawanga mji mdogo wa Lahela ili kuhakikisha wanatoa huduma kwa wananchi wanyonge.

Naye mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya tarime Ndugu. Apoo Castro Tindwa kwa kushirikiana na madiwani wa halmashauli hiyo wameafikiana kuhama haraka kutoka katika halmashauri ya mji wa Tarime na kwenda katika eneo lililopangwa kwa ajili ya halmashauri hiyo ikiwa ni kati ya halmashauri 31 ambazo azipo katika maeneo ya kiutawala.

Hata hivyo halmashauri ya wilaya ya Tarime tayari imeshahamia katika kijiji cha Nyamwaga Kata ya Nyamwaga ndani ya majengo ya ofisi ya tarafa na kijiji kwa muda, wakisubiria kujengwa kwa ofisi zake katika eneo lililotengwa kwa ajili ya makao makuu ya Halmashauri ya wilaya Tarime Nyamwaga.

Katika ziara yake ya kutembelea na kukagua makao mapya ya Halmashauri ya wilaya ya Tarime Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Adam Malima amewapongeza halmashauri ya wilaya ya Tarime kwa kutii agizo la Mhe DK. John Pombe Joseph Magufuri Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuhamia Nyamwanga na kuhakikisha wanatoa huduma kwa wananchi wanyonge,

Wakati wa kikao chake na waheshimiwa madiwani na wakuu wa idara kilichofanyika katika Ukumbi wa shule ya Sekondari JK Nyerere iliyopo Nyamwaga, Mhe. Adam Malima aliwapatia nafasi waheshiwa madiwani kutoa maoni juu ya hatua ya baadhi ya kata za halmashauri ya wilaya ya Tarime kuhamia Halmashauri ya mji wa Tarime, Katika maoni yao waheshimiwa madiwani walimpongeza Mkuu wa Mkoa Mara kwa wazo la kuhamisha kata nane (8) za Sirari,Regicheri,Mwema,Susuni,Bumera,Komaswa,Manga na Kiore kwa lengo la kuwaondolea wananchi wanyonge adha ya umbali wa kufuata huduma makao makuu ya halmashauri ya wilaya ya Tarime yaliyopo Nyamwaga kufuatia jogorafia iliyopo.

Comments

Popular posts from this blog