KAMATI YA BUNGE YAPONGEZA UJENZI KITUO CHA AFYA MURIBA.

www.tarimedc.go.tz
Kamati ya Bunge ya hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) imepongeza ujenzi wa kituo cha Afya Muriba pamoja na huduma zinazotolewa pale ambapo imeitaka Halmashauri ya wilaya ya Tarime kuendelea kutumia Vyema Mapato yake ya Ndani  huku ikitekeleza vyema Miradi ya Maji, Afya , Elimu na Barabara ili kutatu changamoto za Wananchi.
Kauli hiyo imetolewa na Mhe: Abdallah Chikota ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo kipindi walipotembelea kituo cha Afya Muriba kwa ajili ya kukagua Miradi hiyo.

“Sisi kama Kamati tumejilidhisha pia tunafurahishwa na huduma zinazotolewa hapa na changamoto ambazo zinakumba hiki kituo cha Afya tutaenda kuangalia kwenye vitabu kama zimewekwa ili kuzisemea kwa lengo la kuzitatu” alisema Chikota.

Kwa Upande Wake Naibu waziri wa Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe: Mwita Waitara naye alipongeza  Wahudumu Wote katika Kituo cha Afya Muriba kwa huduma nzuri na kusema kuwa baadhi ya wagonjwa wamekuwa wakitoka nje ya wilaya ya Tarime kwa lengo la kwenda kupata matibabu pale baada ya kuboresha Mazingira.
 Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Tarime Mhe: Moses M. Misiwa aliomba kamati hiyo kukumbusha Serikali kuleta Fedha za Ruzuku ili kusaidia kusukuma Maendeleo katika Halmashauri.
“Halmashauri hii ya wilaya  ya Tarime inatekeleza miradi yake kwa kutumia Mapato yake ya ndani tangu 2016 serikali kuu haijawahi kutuletea Ruzuku sasa kama kamati tunaomba ili suala mulifikishe serikalini” alisema Misiwa.







Aidha Wananchi wamebainisha Changamoto mbalimbali mbele ya kamati hiyo huku suala la upatikanaji wa maji safi na salama katika kituo hicho likiibuka,

Comments

Popular posts from this blog